STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 22 Mei 2016

LIGI KUU TANZANIA BARA YAMALIZIKA ,TANGA MAJANGA WAIAGA RASMI VPL MSIMU UJAO.......

 

AZAM FC imeipiku Simba SC kwa kumaliza nafasi ya pili baada ya mechi za mwisho za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo.
 
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, JKT Ruvu imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Simba SC, mabao yake yakifungwa na Abdulrahman Mussa dakika ya kwanza na 30, wakati la Wekundu wa Msimbazi limefungwa na Nahodha Mussa Hassan Mgosi dakika ya 70.

 
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam pia, wenyeji Azam FC wamelazimishwa sare ya 1-1 na Mgambo JKT ya Tanga.

 
Ramadhani Singano ‘Messi’ alianza kuifungia Azam FC dakika ya 60 kabla ya Fully Maganga kuisawazishaia Mgambo dakika ya 72.
Kiungo wa Simba, Abdi Banda akipambana katikati ya wachezaji wa JKT Ruvu leo

Kwa matokeo hayo, Azam FC inamaliza na pointi 64, ikifuatiwa na Simba SC inayomaliza na pointi 62 katika nafasi ya tatu.
 
Yanga SC ambayo ilitwaa ubingwa wa Ligi Kuu wiki mbili zilizopita, leo imemaliza kwa sare ya kufungana mabao 2-2 na wenyeji Majimaji Uwanja wa Majimaji mjini Songea hivyo kufikisha pointi 73.

 
Mechi nyingine za kufunga pazia la Ligi Kuu, wenyeji Toto Africans wamefungwa 1-0 na Stand United Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Coastal Union wamefungwa 2-0 na Prisons 


Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Mbeya City imelazimishwa sare ya 0-0 na Ndanda FC, Mtibwa Sugar wameichapa 2-0 African Sport na Kagera Sugar wameshinda 2-0 dhidi ya Mwadui FC.
 
Kwa matokeo hayo, timu zote za Tanga, Mgambo JKT, African Sports na Coastal Union zinaipa mkono wa kwaheri Ligi Kuu, zikizipisha Ruvu Shooting, Mbao FC na African Lyon.  

 
Mgambo JKT imemaliza na pointi 28, African Sports 26 na Coastal 22. 


       ORODHA YA WAFUNGAJI BORA

PlayerGoals
1Amisi Tambwe21
2Hamisi Kiiza19
3Donald Ngoma17
4Elias Maguli13
5Jerema Juma13

MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM

RnTimuPWDLFAGdPts
1YANGA30227170205073
2Azam FC301810247242364
3SIMBA SC30195645172862
4T. PRISONS30131252822651
5MTIBWA SUGAR30148833211250
6MWADUI FC30118112929041
7STAND UNITED30124142830-240
8MBEYA CITY3098133234-235
9NDANDA FC3071492831-335
10MAJIMAJI FC3098132240-1835
11JKT RUVU3088143139-832
12KAGERA SUGAR3087152434-1031
13TOTO AFRICANS3079142640-1430
14MGAMBO SHOOTING30610142436-1228
15AFRICAN SPORT3075181334-2126
16Coastal Union3057181741-2422


WAKATI HUO; 

BEKI wa kulia, Juma Abdul Jaffar Mnyamani ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa mwezi Aprili, 2016 baada ya kuwashinda kwa kura mshambuliaji Mzimbabwe Donald Ngoma anayecheza naye Yanga SC ya Dar es Salaam na kiungo Hassan Dilunga wa JKT Ruvu ya Pwani.
 
Katika rekodi za Bodi ya Ligi Tanzania Bara (TPLB) iliyoketi Jumamosi Iliyopita, imeonesha kwamba Abdul alicheza mechi zote tano za Ligi Kuu kwa mwezi Aprili ambapo pia aliifungia timu yake bao katika harakati za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2015/16.



Juma Abdul Jaffar Mnyamani (kushoto) ndiye mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara mwezi Aprili  
Rekodi hizo pia zinaonyesha kwamba beki huyo hakuonyeshwa kadi hata moja katika michezo hiyo mitano sambamba na kutoa mchango mkubwa katika michezo aliyoshiriki kwa mwezi Aprili, 2016. Abdul atazawadiwa fedha Sh. 1,000,000 (milioni moja) na wadhamini wa Ligi hiyo, Kampuni ya mahiri ya simu za mkononi ya Vodacom.
 
Uwezo aliouonyesha Abdul ulisababisha Kocha wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa ‘Master’ kumjumuisha katika kikosi chake kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Harambee Stars ya Kenya kadhalika Mapharao wa Misri katika mechi ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Juni 4, mwaka huu.

 
Wachezaji bora wa miezi minne iliyopita ni kiungo Thaban Kamusoko wa Yanga SC (Desemba 2015), beki Shomari Kapombe wa Azam (Januari 2016), Mshambuliaji Mohamed Mkopi wa Tanzania Prisons (Februari 2016) na Shiza Ramadhani Kichuya wa Mtibwa Sugar (Machi 2016).


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox