Mchezo huo ulikuwa sehemu ya maandalizi ya mchezo wa Kundi A Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Mouloudia Olympique Bejaia ya Algeria Jumamosi ijayo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga itakuwa inasaka ushindi wa kwanza siku hiyo baada ya kucheza mechi zote nne za awali bila ushindi, ikifungwa tatu na kutoa sare moja.
Kikosi cha Yanga kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Hassan Kessy, Mwinyi Mngwali, Andrew Vincent ‘Dante’, Vincent Bossou, Said Makapu, Juma Mahadhi, Thabani Kamusoko, Matheo Anthony/Yussuf Mhilu dk62, Obrey Chirwa na Deus Kaseke.
Mtibwa Sugar; Abdallah Makangana, Ally Shomary, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Salim Mbonde, Cassian Ponera, Henry Joseph, Ally Makarani, Ibrahim Rajab 'Jeba'/Vincent Barnabas dk76, Rashid Mandawa/Jaffar Salum dk79, Mohammed Issa/Shaaban Nditi dk53 na Haroun Chanongo/Maulid Gole dk87.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni