STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 23 Mei 2018

ANGALIA ORODHA YA WACHEZAJI WALIOTAJWA KUWANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA VPL, SIMBA YAONGOZA...

Kamati ya Tuzo za VPL, imekamilisha orodha ya awali ya wachezaji 30 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msimu wa mwaka 2017/18, ambayo sherehe zake zitafanyika Juni 23 mwaka huu.

Kila mwezi Kamati ya Tuzo, imekuwa ikitangaza jina la mchezaji aliyefanya vizuri kwa mwezi husika kutokana na vigezo mbalimbali na pia ripoti kutoka kwa makocha waliopo katika viwanja ambavyo ligi hiyo inachezwa.

Wachezaji walioshinda tuzo za mwezi ligi ya msimu huu na miezi yao katika mabano nimshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi (Agosti), beki wa Singida United, Shafiq Batambuze (Septemba) na mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chirwa (Oktoba). Wengine ni kiungo wa Singida United, Mudathir Yahya (Novemba), mshambuliaji wa Mbao FC ya Mwanza, Habibu Kiyombo (Desemba), mshambuliaji wa Simba, John Bocco(Januari), kiungo wa Yanga, Papy Tshishimbi (Februari), mshambuliaji wa  Lipuli, Adam Salamba (Machi) na mshambuliaji wa Majimaji, Marcel Kaheza (Aprili).

Wachezaji hao kila mmoja amepewa zawadi ya tuzo, king'amuzi cha Azam na fedha taslimu sh. Mil. Moja kutoka kwa wadhamini Vodacom.

Hivyo wakati huu tukielekea mwisho wa ligi, leo tunatangaza wachezaji 30 ambao watawania tuzo hiyo, ambao watachujwa na kubaki 10, kisha watabaki watatu ambao ndiyo wataingia fainali ya kuwania tuzo siku ya mwisho.

Wachezaji hao 30 ni

1. Habibu Kyombo (Mbao)

2. Khamis Mcha- Ruvu Shooting

3. Yahya Zayd-Azam

4. Razack Abalora-Azam

5. Bruce  Kangwa-Azam

6. Aggrey Morris -Azam

7. Himid Mao –Azam FC

8. Awesu Awesu –Mwadui

9. Adam Salamba-Lipuli

10. Mohammed Rashid-Prisons

11. Shafiq Batambuze-Singida

12. Mudathir Yahya-Singida United

13. Marcel Kaheza- Majimaji

14. Ditram Nchimbi-Njombe Mji

15. Eliud Ambokile- Mbeya City

16. Shaaban Nditi-Mtibwa

17. Tafadzwa Kutinyu-Singida

18. Ibrahim Ajibu- Yanga

19. Gadiel Michael-Yanga

20. Papy Tshishimbi-Yanga

21. Kelvin Yondani-Yanga

22. Obrey Chirwa-Yanga

23. Aishi Manula-Simba

24. Emmanuel Okwi-Simba

25. John Bocco-Simba

26. Jonas Mkude-Simba

27. Erasto Nyoni-Simba

28. Shiza Kichuya-Simba

29. Asante Kwasi –Simba

30. Hassan Dilunga-Mtibwa

Licha ya Tuzo ya Mchezaji Bora wa mwaka wa ligi, pia kunatolewa tuzo mbalimbali, ambapo kwa mwaka huu tuzo moja imeondolewa na nyingine imeongezwa ikiwa ni katika kuboresha.

Tuzo iliyoondolewa ni ya Mchezaji Bora wa Kigeni na imefanyika hivyo ili kuwapa fursa wachezaji wote kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL badala yakuwatenganisha.

Pia msimu huu imongezwa Tuzo ya Mwamuzi Bora Msaidizi ambayo haikuwepo msimu uliopita, hiyo ni kutokana kuthamini nafasi ya waamuzi wasaidizi.

Kwa mazingira hayo tuzo zitakazotolewa Juni 23, ambapo wadhamini wakuu ni Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom ni hizi zifuatazo:

Bingwa
Mshindi wa Pili
Mshindi wa Tatu
Mshindi wa Nne
 Mfungaji Bora
Timu yenye nidhamu
U20 Player (Tuzo ya Ismail Khalfan)
Mchezaji Bora Chipukizi
Mwamuzi Bora Msaidizi
Mwamuzi Bora
Kipa Bora
Kocha Bora
Goli Bora  
VPL Best Eleven
Mchezaji wa heshima

Zawadi kwa kila kategori pamoja na majina ya wanaowania tuzo ukiacha bingwa, mshindi wa pili, wa tatu, wa nne na mfungaji bora ambao hujulikana kulingana na ligi inavyoendelea zitatangazwa siku za usoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox