Mabingwa wa klabu bingwa Afrika
mashariki na kati Azam FC wametolewa katika mashindano ya kombe la
Mapinduzi baada ya leo kukubali kichapo cha goli 2-1 toka kwa Mafunzo
FC katika mchezo wa mwisho wa kundi B uliochezwa katika uwanja wa Amani
visiwani Zanzibar.
Katika mchezo wa leo Azam FC waliuwanza
mchezo kwa kasi na kutengeneza nafasi kadhaa ambazo zilipotea miguuni
mwa Kipre Tcheche na Allan Wanga.
Katika dakika ya 20 Kipre Tcheche aliandikia Azam FC goli la pili akiunga kona ya Shomari Kapombe na kuipa uongozi Azam FC.
Kuingia kwa goli hilo kuliongeza hali
ya kujiamini kwa wachezaji wa Azam FC huku wakiendelea kupoteza nafsi za
kufunga huku wakiendelea kutawala mchezo.
Katika dakika ya 35 Mafunzo FC
walipeleka shambulio lao la kwanza lngoni mwa Azam FC na kufanikiwa
kuandika goli la kusawazisha katika dakika ya 35 kupitia kwa Rashid
Abdallah.
Kungia kwa goli hilo kuliwarudisha
mchezoni Mafunzo na kuanza kutawala eneo la kati na kupelekea Azam FC
kuanza kutumia mipira mirefu bila mafanikio yoyote ile na kupelekea
kwenda mapumziko wakiwa sare ya goli 1-1.
Kipindi cha pili Mafunzo walirejea na
kasi ile ile na kutibua mipango yote ya Azam FC huku wakipeleka
mashambulizi ya kushtukiza na kupoteza nafsai kadhaaa za kujipatia
magoli.
Katika dakika ya 90 mtokea benchi Sadick
Rajab aliiandikia Mafunzo goli la pili na kupeleka mchezo kumalizika
kwa Mafunzo kuibuka na ushindi wa goli 2-1.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 7 Januari 2016
AZAM FC NA MAFUNZO ZAAGA MAPINDUZI CUP, YANGA, MTIBWA ZATINGA NUSU KIULAINI
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni