MENEJA wa Real Madrid,
Carlo Ancelotti bado anataka kuendelea kuinoa timu hiyo lakini amesema
mustakabali wake utaamuliwa katika mchezo wa mwisho dhidi ya Getafe
Jumamosi hii.
Ancelotti aliingoza Madrid kunyakuwa taji la Ligi ya
Mabingwa Ulaya msimu uliopita, lakini kufuatia kushindwa kunyakuwa taji
la La Liga na kuondolewa katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo
ya Ulaya wiki iliyopita, klabu inafikiria kumtimua na nafasi yake
kuchukuliwa Rafa Benitez.
Pamoja na tetesi hizo za kutimuliwa, Ancelotti
ameonyesha utulivu huku akidai kuwa mustakabali wake ataujua baada ya
mchezo mwisho, ingawa mwenyewe angependa kubakia.
Kocha huyo amesema
bado hajazungumza na klabu kuhusu mustakabali wake hivyo ataenndelea
kuwa kocha mpaka itakapoamuliwa vinginevyo.
Ancelotti aliendelea kudai
kuwa baada ya mchezo wa Jumapili hii au Jumatatu ndio atakaa na
kuzungumzia mustakabali wake na klabu na baadae ndio uamuzi utatoka kama
aondoke au abakie.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni