STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 20 Mei 2015

KOPUNOVIC ANARUDI SIMBA? AMEKUBALI KUPUNGUZA MKWANJA

TAARIFA mpya leo zinasema kocha mkuu wa Simba aliyemaliza mkataba wake, Mserbia Goran Kopunovic amekubali kurejea Dar es salaam kuendelea na kazi ya kuwanoa vijana wa Msimbazi wenye uchu wa mafanikio kuelekea msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Tayari Simba kupitia kwa mwenyekiti wa kamati ya usajili, Zacharia Hans Poppe walithibitisha kuachana na Kopunovic kwasababu ya kutaka dau kubwa la usajili na mashahara mrefu, hivyo kuanza harakati za kusaka kocha mpya.
Kopunovic alitakiwa kutoa jibu kufikia Ijumaa ya wiki iliyopita kama atasaini mkataba mpya au la!, lakini alishindwa kufanya hivyo.
Kopunovic alitaka dola za Kimarekani 50,000 (sawa na Sh. Milioni 100) kama dau la kusaini Mkataba na mshahara wa dola 8,000 (Sh. Milioni 16) kwa mwezi, kiasi ambacho Simba walisema hawawezi kulipa.
Sasa Mserbia huyo amekubali kushuka  dau na atarejea nchini kuanzia juma lijalo kusaini Mkataba mpya na mara moja kuanza maandalizi ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame.

Yuke kocha Mbelgiji Piet de Mol aliyeripotiwa kuja kesho kuwania nafasi ya Kopunovic, atakuja kama kawaida, lakini kutafuta kazi klabu nyingine.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox