STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 19 Mei 2015

MAN WAKUBALI KUMUUZA DE GEA, DAU LAITISHA MADRID

Manchester United wameitaka Real Madrid kulipa dau la usajili la paundi milioni 29 kama wanaitaka saini ya mlinda mlango David De Gea anayeripotiwa kufikia makubaliano binafsi na miamba hiyo ya Hispania.
De Gea amebakiza miezi kumi na minne katika mkataba wake wa sasa na dalili zote za kutimka Old Trafford zimeonekana, lakini Manchester United na Real Madrid bado hazijakubaliana ada ya usajili ya kipa huyo mwenye miaka 24.
Vyombo vya habari vya Hispania vinadai kuwa United wanahitaja euro milioni 40 sawa na paundi milioni 28.6 ili kumuachia kipa huyo wa kimataifa wa Hispania, lakini Real wanataka kumuhusisha katika usajili huo mlinzi wao, Fabio Coentrao.
Mbali na hayo, Man United pia inahusishwa na mpango wa kumsajili nyota wa Real Madrid, Gareth Bale na habari zilizotoka  Hispania leo zinaeleza kuwa winga huyo hatajumuishwa katika usajili wa De Gea.
Wakati huo huo ripoti zinasema kuwa De Gea atatuta Bernabeu hata kama mlinda mlango chaguo la kwanza kwa sasa, Iker Casillas ataendelea kuwepo au hapana.

Hatima ya Casillas katika mji wa Madrid ipo shakani kutokana na kushuka kwa kiwango chake na kusababisha agombanie nafasi ya kuanza na Keylor Navas

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox