STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 27 Mei 2015

MAOFISA SITA WA FIFA AKIWEMO MAKAMU WA RAIS WAKAMATA KWA RUSHWA NCHINI USWISS


BEPARI BLATTER.
Maofisa sita wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) wamekamatwa jijini Zurich kwa tuhuma za rushwa.


Maofisa hao akiwemo Makamu wa Rais wa Fifa, Jeffrey Webb wametiwa nguvuni na Jeshi la Polisi la Uswis, leo saa 12 alfajiri.
 
Maofisa hao walikamatwa katika hoteli moja ya kifahari na kutolewa huku wakiwa wamefunikwa kwa shuka na wafanyakazi wa hoteli hiyo ili wasipigwe picha.
 
WAKIINGIA KWENYE GARI LA POLISI.
Inaelezwa wanatuhumiwa kupokea rushwa ili kutoa nafasi kwa mashindano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi na 2022 yatakayofanyika nchini Qatar kufanyika katika nchi hizo.
Pia imeelezwa memba wengine 10 wa kamati ya utendaji ya Fifa watahojiwa.
MAKAMU WA RAIS WA FIFA AMBAYE NI RAIS WA CONCACAF, NAYE AMTIWA MBARONI.

Madai hayo yameongeza kwamba maofisa hao wanaaminika kuchota rushwa hadi ya dola milioni 100 kwa ajili ya kuizipa nchi hizo nafasi.

Msemaji wa Fifa, Walter de Gregorio amesema licha ya maofisa hao kutiwa mbaroni, komgamano la kesho Ijumaa kuhusiana na uchaguzi wa Rais wa Fifa litaendelea kama kawaida.
Rais wa sasa wa Fifa, Sepp Blatter ndiye anayepewa nafasi kubwa kushinda kwa muhula wa tano mfululizo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox