MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Uruguay na klabu ya Paris Saint-Germain, Edinsoni Canavi ameomba radhi baada ya kudai kuwa Jamaica in ngumu kupambana nayo kama zilivyo timu zote za Afrika.
Nyota huyo wa zamani wa Napoli alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na wana habari kuelekea mchezo wao wa Jumamosi wa Copa America dhidi nchi hiyo inayotoka upande wa mataifa ya Caribbean.
Kauli hiyo ambayo wengi waliichukulia kama ya kibaguzi ilimfanya Cavani kuomba radhi haraka katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter akidai alikuwa akifananisha aina ya uchezaji wa Jamaica na baadhi ya timu za Afrika na sio vinginevyo kama watu wanavyotafsiri.
Nyota huyo aliomba radhi kwa watu wa Jamaica kwa kauli yake hiyo kueleweka vibaya na alikuwa hana nia yeyote mbaya. Uruguay ambao ndio mabingwa watetezi wa michuano hiyo wanatarajiwa kutupa karata yao ya kwanza katika michuano hiyo kesho wakichuana na Jamaica.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni