BAADA
ya wa klabu ya Simba umesema upo tayari kumuuza kiungo wao
mshambuliaji, Ramadhan Singano ‘Messi’ kwenye klabu ya Azam FC ambayo
inasemekana ndiyo inamshawishi mchezaji huyo ili iweze kumsajili kwa
ajili ya msimu ujao.
Timu ya Azam FC ni moja kati ya klabu zinazowania saini ya kiungo
huyo mwenye kasi ndani ya uwanja kwa ajili ya kumsajili katika usajili
wa msimu huu wa Ligi Kuu Bara.
Msemaji wa Simba Haji Manara, ameiambia Goal kuwa
wamepata taarifa hizo za mchezaji kufanya mazungumzo na Azam na hivyo
wao wameona ni vyema wakamuachia mchezaji huyo aondoke kwa sababu tayari
ameonekana ana mapenzi na klabu hiyo badala ya Simba.
“Tumegundua kuwa, katika sakata hili linaloendelea kati yetu na Messi
zipo baadhi za timu zinahusika katika kumshawishi mchezaji huyo kwa
kulazimisha kuwa mkataba umeisha wakati siyo ukweli sasa tunawataka Azam
waje mezani tuzungumze kama kweli wanamtaka ‘Messi’ na pia wanatakiwa
kujua kwamba kitendo cha kuzungumza na mchezaji huyo wakati bado
anamkataba wa mwaka mmoja na Simba ni kosa la kisheria,”amesema Manara.
Manara amesema thamani ya Messi ni Tsh. Milioni 200 hivyo kama Azam
wapo tayari kutoa kiasi hicho cha pesa wanawakaribisha ili kuwenda
kumaliza mzozo huo ambao umechukua nafasi kubwa kwenye vyombo vya habari
tangu uliopoanza wiki mbili zilizopita.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Alhamisi, 4 Juni 2015
HATIMAYE SIMBA WATAJA DAU LA MESSI
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni