STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 9 Juni 2015

ILE KESI YA SIMBA NA MESSI HII HAPA HUKUMU YAKE.....

Leo hii ndio siku ambayo sakata la Ramadhan Singano a.k.a Messi lilikua linasikilizwa kwenye ofisi za TFF ambapo pande mbili zilikutana chini ya TFF.
Baada ya kikao kirefu muafaka uliofikiwa chini ya TFF ni kwamba kuvunjwa kwa mikataba yote miwili ambayo inatofautiana. kikao kimeamua kwamba mkataba wa alionao Messi uvunjwe na mkataba walionao Simba uvunjwe waingie makubaliano mapya
Upande wa Singano haujakubaliana na maamuzi hayo kwasababu unamtaka yeye akubaliane na Simba tena. Lakini kwa mujibu wake ni kwamba anatakiwa kuwa huru kama mkataba umevunjwa na sio kukubaliana upya na Simba. Singano anataka kuwa mchezaji huru ndio aamue mwenyewe kama kuongea na Simba au club nyingine.

Kama TFF wamewataka Singano na Simba kuzungumza upya kwasababu mikataba yote imefutwa, maana yake wakishindwana, Singano anachukua hamsini zake na sio lazima akubali kuendelea kuichezea Simba.

Wakati huo huo, mtandao huu umefahamishwa kuwa, Katibu mkuu wa TFF, Mwesigwa amemuandikia barua Singano ambayo nakala yake amechukua mwenyekiti wa SPUTANZA, Bwana Kisoky  ikithibitisha maamuzi yaliyochukuliwa  na kuwa ushidi wa maazimio ya kikao hicho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox