KLABU ya Juventus inatarajiwa kutenga kitita cha paundi milioni 10, kwa ajili ya kumuwani mshambuliaji wa Manchester United Robin van Persie.
Mabingwa hao wa Italia wanajipanga kutafuta mbadala wa Carlos Tevez na wanaona chaguo sahihi kuziba nafasi hiyo atakuwa in Van Persie.
Tevez anategemewa kuondoka majira haya ya kiangazi baada ya mafanikio aliyopata toka atue kuitumikia klabu hiyo marufu kama Vibibi Kizee vya Turin.
Klabu ya Paris Saint-Germain imeonyesha nia ya kumtaka Tevez, lakini mwenyewe pia anafikiria kurudi nchini kwao Argentina mahali alipoanzia soka katika klabu ya Boca Juniors.
Sasa rais wa Juventus Giuseppe Moratta anaataka kumchukua Van Persie ambaye anaonekana kutotulia kutokana na kuwa chini ya kiwango msimu uliopita jambo ambalo lilichangiwa na majeruhi yaliyokuwa yakimuandama.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni