KLABU ya Liverpool, imethibitisha kuwa tayari wameshanasa saini ya mshambuliaji wa Burnley Danny Ings.
Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza, ameshamaliza mkataba wake na Burnley na anatarajiwa kutua Anfield Julai mosi baada ya kufanyiwa vipimo vya afya.
Ings mwenye umri wa miaka 22, amefunga mabao 11 katika Ligi Kuu msimu huu lakini hakuweza kusaidia timu yake hiyo kutoshuka daraja. Nyota huyo wa zamani wa Bournemouth yuko katika kikosi cha Uingereza cha vijana chini ya umri wa miaka 21 kea ajili ya michuano ya ubingwa ya Ulaya baadae mwezi huu huko Jamhuri ya Czech.
Ings anakuwa mchezaji wa pili kusajiliwa na Liverpool baada ya James Milner kujiunga nao akitokea Manchester City wiki iliyopita.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni