MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho amebainisha kuwa klabu hiyo itaingia sokoni katika usajili huu wa majira ya kiangazi kutafuta mshambuliaji mpya. Wiki iliyopita kulizuka tetesi kuwa Mourinho alikuwa akitaka kumsajili Radamel Falcao ambaye ameshindwa kung’aa katika Ligi Kuu toka alipochukuliwa kea mkopo na Manchester United kiangazi mwaka jana.
Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia tayari amesharejea katika klabu yake ya Monaco baada ya United kuamua kutomnunua pamoja na kuwa na nafasi ya kufanya hivyo. Akihojiwa Mourinho amesema wanataka kununua mshambuliaji kwasababu wanahitaji kuwa na washambuliaji watatu walio katika kiwango bora.
Hata hivyo, Mourinho hakuweka wazi na mshambuliaji yupi anayemuhitaji na kudai kuwa wana chaguo zaidi ya moja.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni