RUFANI iliyokatwa na Lionel Messi dhidi ya tuhuma za ukwepaji kodi imetupiliwa mbali na mahakama ya jiji la Barcelona na sasa nyota huyo wa kimataifa wa Argentina atasimama kujibu tuhuma hizo.
Messi na baba yake ambaye pia ndio wakala wake, Jorge Messi wanatuhumiwa kukwepa kodi inayokadiriwa kufikia euro milioni 4.1 kati ya mwaka 2006 na 2009.
Inatuhumiwa kuwa haki za kutumia picha ya Messi ziliuzwa na Jorge kea kutumia kampuni kutoka nchi kama Belize na Uruguay ili kukwepa majukumu ya kodi Hispania.
Jaji wa mahakama ya Gava karibu na Barcelona alibainisha Octoba mwaka jana kuwa Messi mwenye umri wa miaka 27 anaweza kukabiliwa na kesi kuhusiana na tuhuma hizo bila kujali kama ana hatia au la.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni