MENEJA wa Atletico Madrid, Diego Simeone amebainisha kuwa klabu hiyo imefanya mawasiliano na wakala wa mshambuliaji wa Juventus Carlos Tevez.
Mshambuliaji huyo amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wake jijini Turin na ameshindwa kufikia makubaliano juu ya kuongezwa mkataba mpya.
Matokeo hayo yanafanya Atletico na vilabu kadhaa kuanza kumfukuzia nyota huyo na Simeone amekiri kuwa angependa kufanya kazi na Tevez ambaye ana umri wa miaka 31.
Akihojiwa Simeone amesema ukweli in kwamba hajafanya mazungumzo yeyote na tevez lakini klabu inawasiliana na wake na kuongeza kuwa in jambo zuri kuwa na mchezaji kama Tevez.
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa juhudi za Tevez katika ufungaji zinamfanya kuwa mchezaji ambaye atafaa kuimarisha kikosi chake kea ajili ya msimu ujao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni