STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 11 Juni 2015

TAARIFA ILIYOTOLEWA NA TIMU YA SIMBA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MESSI

Simba Sports Club
Taarifa kwa vyombo vya habari
Kikao cha kamati ya utendaji ya club ya simba kilichokutana jana tarehe 10/06/2015, pamoja na mambo mengine kilijadili suala la mchezaji wa Simba Ramadhan Yahya Singano na kuamua yafuatayo:

Kwa kuwa Mchezaji Ramadhan Yahya Singano alivunja makubaliano yaliyoamuliwa katika kikao cha pamoja kati ya club ya Simba, mchezaji mwenyewe, Sputanza na secretarieti ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ya kutozungumzia yaliyojadiliwa na kupendekezwa kwenye kikao kwa kuyazungumza kwenye vyombo vya habari kwa kusema yeye ni mchezaji huru.

Klabu ya simba imeamua kutokufanya mazungumzo na mchezaji huyo kwa sasa kwa kuwa bado ina mkataba naye ambao utaisha 01/07/2016. 

Hata hivyo Klabu itakuwa tayari kufanya naye mazungumzo pindi muda mwafaka utakapofika kwa mujibu wa kanuni na taratibu za mikataba.

Ni matarajio yetu mchezaji Singano ataheshimu maamuzi hayo na mkataba ambao pia upo TFF na kwenye mtandao TMS.


Imetolewa na 
Evans Aveva
Rais 
Simba Sports Club

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox