UTOAJI zabuni ya maandalizi ya Kombe la Dunia mwaka 2026 umeahirishwa kufuatia madai ya ufisadi katika utoaji wa zabuni wa maandalizi ya michuano hiyo mwaka 2018 na 2022.
Katibu mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFAJerome Valcke amesema kuwa ni sio suala la busara kuanza mpango huo katika mazingira yaliopo.
Kura ya kumtafuta atakayeandaa Kombe la Dunia 2016 inatarajiwa kufanyika jijini Kuala Lumpur Mei mwaka 2017.
Marekani ndio wanapewa nafasi kubwa kuandaa michuano hiyo lakini Canada, Mexico na Colombia pia zimewasilisha ombi la kutaka kuandaa.
Urusi na Qatar walichaguliwa kuandaa michuano ya mwaka 2018 na 2022 kupitia kura ya siri iliopigwa na wanachama wakuu wa FIFA wapatao 22 Desemba mwaka 2010. Lakini viongozi wa mashtaka nchini Uswizi wanachunguza madai ya ufisadi yanayozunguka zabuni hizo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni