ALIYEKUWA makamu wa rais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Jack Warner, ameituhumu Marekani kwamba inafuatilia mashtaka ya rushwa dhidi ya maafisa waandamizi wa shirikisho hilo kwa sababu imeshindwa kuwa mwenyeji wa kombe la dunia la mwaka 2022.
Akiandika katika gazeti ambalo analolimiliki huko Trinidad na Tobago, bwana Warner amesema tuhuma hizo dhidi yake na wengine kumi na tatu zinaonyesha kwamba Marekani inaegemea upande mmoja.
Akiandika katika gazeti lake linaloitwa Sunshine, Warner ambaye makanusha tuhuma zote zinazomkabili amesema mashtaka ya Marekani dhidi yake kuwa ni uonevu na yaliyoegemea upande mmoja.
Warner amesema Marekani ambayo inajifanya kuwa ni polisi wa dunia, imehamasika kuchukua hatua hiyo baada ya kushindwa kuwa mwenyeji wa mashindano ya kombe la dunia ya mwaka 2022.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni