MSHAMBULIAJI nyota wa timu ya taifa ya wanawake ya Brazil, Marta amekuwa mfungaji anayeongoza katika historia ya Kombe la Dunia baada ya kufunga bao lake la 15 katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata dhidi ya Korea Kusini.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29, alifunga bao hilo kea njia ya penati na kumfanya kuipita rekodi iliyokuwa ikishikiliwa na mshambuliaji wa zamani wa Ujerumani Birgit Prinz.
Nyota mwingine wa Brazil, Formiga mwenye umri wa miaka 37 alifunga bao la kuongoza na kumfanya kuwa mchezaji aliyefunga bao akiwa na umri mkubwa zaidi kat6ika historia ya michuano hiyo ya wanawake.
Ushindi unaifanya Brazil kuongoza kundi E baada ya Hispania na Costa Rica kutoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni