KOCHA wa klabu ya Queretaro, Victor Manuel amebainisha kuwa timu hiyo inapanga kumuacha nyota wa soka wa kimataifa wa Brazil, Ronaldinho.
Ronaldinho ambaye toka amewasili nchini Mexico amekuwa akiingia katika migogoro ya hapa na pale na kocha huyo, ameshindwa kupata namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza.
Akihojiwa kocha huyo amesema amekuwa hana msaada katika kikosi chake ndio maana wanafikiria kumuacha msimu ujao.
Manuel aliendelea kudai kuwa kimasoko nyota huyo anafanya vyema nab ado ana ubora wa hali ya juu lakini wao wanahitaji mchezaji anayeweza kuwasaidia pande zote yaani kimasoko pamoja na uwanjani.
Ronaldinho amefunga mabao nane katika mechi 25 alizocheza toka alipowasili akitokea Atletico Mineiro mwaka 2014.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni