KASHFA nzito iliyolikumba Shirikisho la Soka Duniani-FIFA imefanya kuandaliwa mkutano wa kipekee wa kamati ya utendaji Julai mwaka huu kujadili tarehe ya uchaguzi kwa ajili ya kuziba nafasi ya rais Sepp Blatter alitangaza kuachia ngazi wiki iliyopita.
Katika taarifa yake FIFA imedai kuwa hakuna muda rasmi ulioamuliwa mpaka kuelekea katika mkutano huo lakini wapekenyuzi wa mambo wanadai kuwa uchaguzi unaweza kufanyika Desemba 16 mwaka huu.
Blatter alitangaza kujiuzulu wadhifa wake huo Jumanne iliyopita ikiwa zimepita siku nne toka alipochaguliwa tena kuliongoza shirikisho hilo jijini Zurich. Hata hivyo Blatter anataka kuendelea kushikilia madaraka hayo mpaka hapo mbadala wake atakapochaguliwa na anataka kuongoza nguvu ya kulisafisha shirikisho hilo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni