Pamoja na Real Madrid kuchapwa mabao 4-0 na
Barcelona lakini nyota wake Cristiano Ronaldo anaweza kuingia matatani kwa
kufungiwa mechi kadhaa au kupigwa faini.
Imebainika Ronaldo, alimtwanga kwa kiwiko beki
wa wa Barcelona, Dani Alves wakati wa mechi hiyo ya jana kwenye Uwanja wa
Santiago Bernabeu.
Lakini inaonekana Ronaldo alikuwa mjanja sana kwani pamoja na kumtwanga Alves, mwamuzi David Fernández Borbalán hakuona na badala yake alimlamba kadi ya njano beki huyo kwamba alimsukuma Ronaldo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni