STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 4 Desemba 2015

DANI ALVES ADAI RONALDO HAKUSTAHILI KUWEPO KATIKA ORODHA YA MWISHO YA BALLON D'OR MWAKA HUU.

BEKI wa Barcelona, Dani Alves amesisitiza Cristiano Ronaldo hakustahili kuwepo katika orodha ya mwisho ya wachezaji watatu watakaogombea tuzo ya Ballon d’Or na kudai kuwa Neymar amekuwa mchezaji wa pili bora duniani baada ya Lionel Messi. 
 
Wote wawili Messi na neymar wametajwa katika orodha hiyo ya mwisho sambamba na nyota huyo wa Real Madrid ambaye amefunga mabao 16 katika mechi 18 za mashindano yote alizochez msimu huu. 
 
Pamoja na hayo, Alves hadhani kama Ronaldo alistahili kuwepo katika kinyang’anyiro hicho ambacho mshindi wake atajulikana Januari mwakani. 
 
Alves amesema Messi anaongoza kwasababu ya uwezo wake mchezoni na kwasasa anayemfuatia kwa ubora ni Neymar. 
 
Beki huyo wa kimataifa wa Brazil aliendelea kudai kuwa Ronaldo hakustahili kuwepo kabisa katika orodha hiyo kwani haiangalii suala la ufungaji pekee.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox