STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 5 Desemba 2015

GUARDIOLA AKANUSHA TETESI ZA KWENDA MADRID.

MENEJA wa Bayern Munich, Pep Guardiola amekanusha tetesi kuwa anaweza kujiunga na Real Madrid kama akiondoka katika klabu hiyo majira ya kiangazi mwakani. 
 
Mkataba wa miaka mitatu wa Guardiola kwa mabingwa hao wa Ujerumani unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu na klabu hiyo inatarajiwa kutangaza uamuzi wake kama ataendelea kubakia huko. 
 
Kocha huyo wa zamani wa Barcelona amekuwa akihusishwa kwa karibu na tetesi kwenda Ligi Kuu huku Manchester City na Manchester United zikitajwa kumuwania. 
 
Lakini taarifa zilizotolea hivi karibuni na vyombo vya habari vya Hispania zimedai kuwa Madrid imetuma watu wake kuona kama Guardiola atapenda kutua Santiago Bernabeu. 
 
Akiulizwa kuhusu suala hilo, Guardiola alikanusha na kuongeza kuwa hadhani kama anaweza kuendana na klabu hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox