STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 26 Desemba 2015

LEICESTER CITY ITARUDIA YA MTIBWA SUGAR..?

 Tokeo la picha la leicester city  fc
 KUNA msemo unaosema duniani wawili wawili. Msemo huu umeonekana kukubalika kwa jamii zote kutokana na jinsi mambo yanayotokea duniani kila kukicha.

Achana kwa kufanana kwa vitu ambavyo vinaweza kutengenezwa na binadamu, hapa msemo huu unagusa kile kinachopangwa na Mungu.

Unaweza kukuta watu wakifanana licha ya kutokuwa ndugu na mifano mingine mingi kama hiyo. 

Katika Ligi Kuu ya England ‘Premier’, kuna timu inaitwa Leicester City, mwanzoni mwa msimu huu timu hii haikuwa ikitajwa sana wala kupewa nafasi ya kuja kutikisa vigogo katika Premier, lakini kwa sasa imekuwa midomoni mwa watu wengi kutokana na kile inachokifanya. 


Timu za Arsenal, Manchester United, Manchester City, Chelsea na hata Liverpool, ndizo zilikuwa zikipewa nafasi kubwa sana ya kufanya vizuri mpaka kufikia siku ya Sikukuu ya Krismasi.
 Tokeo la picha la leicester city  fc

Imekuwa kawaida kwa timu hizo kujiwekea malengo hayo huku zikiamini hiyo ni njia mojawapo ya kujitengenezea mazingira ya kutwaa ubingwa.

 Leo ndiyo Krismasi, na ukiangalia msimamo wa ligi hiyo, utaikuta Chelsea ipo nafasi ya 15, Liverpool ya tisa, Machester United ya tano, Manchester City inakamata nafasi ya tatu huku Arsenal ikiwa ya pili, kwenye ile nafasi ambayo timu hizo zimekuwa zikiilenga, wapo vijana wa Muitaliano, Claudio Ranieri, Leicester City. 

Leicester iliyoanzishwa miaka 131 iliyopita, inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 38 ambazo ni mbili zaidi ya Arsenal. Mbali na kuongoza ligi, pia straika wao tegemezi, Jamie Vardy anaongoza kwa ufungaji akiwa amefunga mabao 15.

Vardy ambaye anaonekana kuwa mwiba kati ya mastraika wa timu zote 20 za ligi hiyo, hivi karibuni alivunja rekodi ya gwiji wa zamani wa, Manchester United, Ruud van Nistelrooy. Rekodi hiyo ni ile ya kufunga mabao kwenye mechi 11 mfululizo.
 Tokeo la picha la VARDY

 Vardy yeye amefikisha mechi 12 akifunga mfululizo. Leicester ama unaweza kuiita Jeshi la Bluu kama inavyojulikana kwa jina lake la utani, inaendelea kupambana na vigogo lakini hali kama hiyo inatukumbusha msimu uliopita katika Ligi Kuu Bara.

 Tokeo la picha la VODACOMLEAGUE TANZANIA
Ligi Kuu Bara ambayo msimu uliopita ilikuwa inazihusisha timu 14, Yanga ndiyo ilikuwa bingwa ikifuatiwa na Azam, lakini tangu kuanza kwa ligi hiyo mpaka ilipofika Januari, mwaka huu wakati ligi imesimama kupisha michuano ya Kombe la Mapinduzi, Mtibwa Sugar ndiyo ilikuwa ikishikilia usukani.
 Tokeo la picha la KOMBE LA MAPINDUZI
 Kila mmoja alianza kuwaza safari ya ubingwa kwa Mtibwa inaelekea vizuri baada ya kufanya hivyo miaka miwili mfululizo, 1999 na 2000.


 Lakini ligi ilipoendelea baada ya Kombe la Mapinduzi kumalizika, kibao kikageuka, Mtibwa ikajikuta inaanza harakati za kujikwamua kushuka daraja, kwa bahati nzuri haikushuka, ilimaliza msimu ikiwa nafasi ya saba.

Kinachozifelisha timu nyingi duniani kote, ni kutokana na wachezaji wao tegemezi kupata majeraha ya muda mrefu. Hicho ndicho kilichovuruga mipango ya vijana wa beki wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Maxime, timu ya Mtibwa Sugar.
 Tokeo la picha la mtibwa sugar
 
Katika wachezaji tegemezi wa Leicester, huwezi kuacha kumtaja Riyad Mahrez na Vardy ambao wamekuwa wakicheza kila mechi, na endapo mmoja wao ama wote wawili wakija kupata majeraha yatakayowaweka nje kwa muda mrefu, bila shaka anguko la timu hiyo litatokea.

Hali kama hiyo imekuwa ikiisumbua mara kwa mara Arsenal na ni wazi inajulikana inafeli kutokana na kukumbwa na lundo la wachezaji majeruhi katika wakati mgumu. Bado mechi 21 kumaliza msimu huu wa Premier, je, Leicester itaweza kuhimili kasi ya vigogo wa ligi hiyo au ndiyo itakuwa hadithi ya Mtibwa msimu uliopita! Tusubiri tuone mwisho wao.

IMEANDIKWA NA:
             OMARY SULTAN MDOSE

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox