MABINGWA watetezi, Simba SC wamepangwa Kundi A katika Kombe la Mapinduzi 2016 pamoja na URA ya Uganda, Jamhuri ya Pemba na JKU ya Unguja.
Katika ratiba iliyotolewa leo na Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), mabingwa wa Bara, Yanga SC wamepangwa kundi moja, B pamoja na mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, Mtibwa Sugar ya Morogoro na Mafunzo ya Zanzibar.
Simba SC itafungua dimba na Jamhuri Januari 2, 2016 mchezo ambao utatanguliwa na mechi kati ya JKU na URA Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni