STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 30 Desemba 2015

SAMATTA AFAFANUA SUALA LA MKATABA WAKE NA GENK, ATIMBA KWA WAZIRI NAPE.............................


Pamoja na meneja wake, Jamal Kisongo kusema tayari Mbwana Samatta amesaini mkataba wa awali wa miaka miwili na Genk, mshambuliaji huyo amesema bado wanaendelea kuwasubiri TP Mazembe.

“Bado tunasubiri Genk wamalizane na Mazembe, huwezi kumsainisha mchezaji wa timu nyingine mkataba. Lakini mimi nimeshamalizana na Genk kwa maana ya makuabaliano, suala la mkataba litafuatia,” alisema Samatta.

Samatta anatarajia kuondoka nchini kwenda Nigeria katika tuzo za mchezaji bora wa Afrika yeye akiwa anawania tuzo ya wachezaji wanaocheza ndani ya bara la Afrika.

Samatta anapewa nafasi ya kutwaa tuzo hiyo kutokana na kuisaidia TP Mazembe kutwaa ubingwa wa Afrika pamoja na yeye kuibuka mfungaji bora.


Tamasha maalum la tuzo hizo limepangwa kufanyika Januari 7 jijini Lagos, Nigeria ikiwa ni siku mbili tu baada ya Samatta kutua nchini humo.
 
Wakati huohuo  
 
Serikali imesema ipo bega kwa bega na mshambuliaji nyota wa Taifa Stars, Mbwan Samatta kokote aendako.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amemuambia Samatta leo mbele ya waandishi wa habari kwamba Serikali itamuunga mkono kokote aendako.


“Tuko na wewe pamoja kokote uendako, pia ninakupongeza kwa kuwa sehemu ya changamoto kwa wengine kutokana na mafanikio uliyofikia,” alisema Nape.

Samatta ameishakubaliana na klabu ya Genk ya Ubeligiji na sasa limebaki suala la Genk kumalizana na TP Mazembe ili Januari shughuli za uhamisho zifanyike.


Samatta alitembelea ofisi za Waziri Nape na kusema alifika hapo kwa ajili ya kupata baraka kabla ya kwenda kokote.

“Nimekuja kupata baraka, baraka za wazazi ni jambo muhimu sana kwa mtoto, ndiyo maana nipo hapa,” alisema Samatta ambaye alielezea kuhusiana na mkataba wa Genk.

“Suala la kusaini bado, ila makubaliano yote yako safi. Nasubiri wao wamalizane na TP Mazembe baada ya hapo mambo mengine yatafuatia,” alisema Samatta.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox