STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 11 Februari 2016

STORI KUBWA TATU NCHINI UINGEREZA KUHUSU MANCHESTER UNITED,SUNDELAND NA WEST HAM UNITED......................

 http://orig05.deviantart.net/12ac/f/2014/148/a/0/manchester_united_wallpaper_by_jamesg2498-d7k264t.png

Timu ya Manchester United iko mbioni kuvunja rekodi ya Uingereza kwa kuwa klabu ya kwanza kabisa kuvuna mapato ya zaidi ya pauni nusu bilioni kwa mwaka mmoja.

Timu hiyo imezidi kuimarika Kibiashara na wametangaza mapato yao kwa mwaka yatagonga pauni milioni 500 hadi 510 kitu ambacho hakuna klabu yeyote ya Uingereza imewahi kufikisha.

 

Mapato kwa robo ya pili ya mwaka yamepanda na kufikia pauni milioni 133.8 ikiwa ni ongezeko la asilimia 26.6 kutoka ya mwaka uliopita wa fedha.

 

Mapato kutokana na matangazo yamepanda kwa asilimia 31.3 na yale ya udhamini kwa robo ya pili ya mwaka yamepanda kwa pauni milioni 1.6 na kufikia pauni milioni 37.4.

Pia, Man United sasa wapo kwenye uvumi mkubwa kuwa meneja wao, Louis van Gaal, atabadilishwa mwishoni mwa Msimu na nafasi yake kuchukuliwa na Jose Mourinho.

                                   SUNDERLAND

 

Klabu ya Sunderland imefuta Mkataba na Mchezaji wake Adam Johnson mara tu baada ya mchezaji huyo kukiri Makosa Mawili Mahakamani kwenye Kesi iliyomkabili ya kuwa na uhusiano wa ngono na Binti wa chini ya Miaka 16.

Johnson, mwenye umri wa miaka 28, aliishtua timu yake baada ya kukiri Kosa moja Mahakamani katika Kesi yake tofauti na kile walichotegemea ambapo sasa amekubali kumrubuni Binti wa Miaka 15 na kumbusu lakini kukana kufanya nae ngono.

Meneja wa Sunderland, Sam Allardyce, alithibitisha kuwa Johnson hatakuwemo kwenye Kikosi cha Timu yao ambacho Jumamosi kitacheza na Manchester United.
 


Mkataba wa winga huyu umevunjwa mara tu baada ya Kampuni ya Kutengeneza Vifaa vya Michezo, Adidas, kuamua kuvunja Mkataba wa Udhamini na Mchezaji huyo.

Kesi ya Johnson itaendelea Bradford Crown Court Ijumaa ambako anakabiliwa na Jumla ya Mashitaka Manne ambayo yote awali aliyakana.

Kwa makosa ambayo ameyakiri, Mchezaji huyo sasa ana hatari ya kufungwa si zaidi ya Miaka Miwili na Nusu.

Johnson, alizaliwa mjini Sunderland alianza kucheza soka katika timu ya Middlesbrough kisha akajiunga na Manchester City kabla ya kusajiliwa na Sunderland, kwa dau la pauni milioni 10 mwaka 2012.

                             WEST HAM UNITED

 



Kiungo mshambuliaji wa timu ya soka ya West ham, Dimitri Payet amesani mkataba mpya wa miaka mitano na timu yake.

Payet mwenye umri wa miaka 28 alijiunga na Wagonga nyundo hao wa London msimu uliopita akitokea timu Marseille kwa dau la zaidi ya pauni milioni 10.

Mapema wiki hii klabu yake ilizikataa taarifa zilizosambaa kuwa mchezaji huyo anataka mkataba mpya, huku mkataba wake wa kwanza pia ukiwa ni miaka mitano.

 http://cdn.images.express.co.uk/img/dynamic/galleries/x701/64588.jpg

Mchezaji huyu wa kimataifa wa Ufaransa amezifumania nyavu mara 6 katika michezo 22 aliyocheza na kuiweka West Ham katika nafasi ya sita ya msimamo wa ligi kuu ya England.

David Sullivan, mmiliki wa timu hiyo amesema "tutafanya chochote kuwabakiwa wachezaji wetu wazuri na Payet ni mchezaji mzuri."

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox