Jurgen Klopp amefanikiwa kufikisha Liverpool kwenye hatua ya fainali ya Europa League kwenye msimu wake wa kwanza tangu ajiunge na klabu hiyo baada ya kuifunga Villarreal kwenye mchezo wa maruadiano wa nusu fainali.
Akipoteza kwa bao 1-0 kwenye mchezo wa ugenini, Liverpool walianza kupata matumaini kwenye mchezo wa Alhamisi usiku baada ya Bruno Soriano kujifunga na kufanya matokeo ya jumla kuwa 1-1.
Daniel Sturridge akamalizia kazi nzuri ya Roberto Firmino baada ya mchezaji wa Villareal Victor Ruiz kutolewa kwa kadi nyekundu, Adam Lallana alipigilia msumari wa mwisho kwa kufunga bao la tatu usiku wa Alhamisi na kufanya mambo kuwa 3-0 huku matokeo ya jumla (aggregate) yakiwa ni Liverpool 3-1Villarreal.
Klopp ambaye alichukua timu hiyo kutoka kwa Brendan Rodgers
mwezi Oktoba mwaka jana ameshaifikisha Liverpool katika fainali mbili
huku ya kwanza ikiwa katika kombe la ligi ambapo walipoteza dhidi ya
Manchester City. Kwa matokeo hayo watakutana katika fainali na mabingwa
watetezi Sevilla mjini Basel Mei 18 jumatano katika uwanja St Jakob-Park Stadium, Basle .
Sevilla walifika fainali kwa kuwacharaza Shakhtar Donetsk kwa matokeo ya jumla ya 5-3.
Mambo muhimu kufahamu
- Liverpool ilishindwa kufunga goli kwenye mchezo mmoja kati ya michezo 21 ya Europa League (Liverpool 0-0 Braga mwezi December 2010)
- Daniel Sturridge amefunga kwenye mechi nne kati ya tano zilizopita alizocheza kwenye uwanja wa Anfield kwenye mashindano yote.
- James Milner ndiye mchezaji mwenye assists nyingi (14) ndani ya Liverpool msimu huu akifuatiwa na Roberto Firmino (9)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni