Klabu ya West Ham United iliaga
uwanja wake wa nyumbani wa Upton Park kwa kuvuruga juhudi za Manchester
United za kutaka kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Jumanne.
Kwenye mechi hiyo ya kusisimua, West Ham walichomoza na ushindi wa 3-2.
Vijana wa Louis van Gaal walifahamu kwamba ushindi dhidi ya klabu hiyo na baadaye ushindi dhidi ya Bournemouth vingewahakikishia nafasi katika ligi kuu ya klabu Ulaya.
Lakini kushindwa kwao kuna maana kwamba Manchester City, walio nambari nne, wamo alama nne mbele yao kabla yao kucheza mechi ya mwisho dhidi ya Swansea City.
West Ham walitangulia kupitia bao la Diafra Sakho kipindi cha kwanza, lakini Antony Martial aliwasawazishia Red Devils kwa bao dakika ya 51 na kisha akawaweka kifua mbele dakika ya 72.
West Ham, hata hivyo, walijikwamua kwa kufunga mabao mawili ya kichwa katika kipindi cha dakika nne kupitia Michail Antonio na Winston Reid aliefunga goli la mwisho katika uwanja huo ikiwa ni kumbukumbu kubwa katika historia yake na klabu kwa ujumla.
West Ham bado wana nafasi ya kumaliza katika nambari tano.
Wamo alama moja nyuma ya Manchester United na watazuru Stoke Jumapili.
Manchester United, watakuwa wenyeji wa Bournemouth, mechi ambayo watahitajika kushinda kujiimarishia uwezekano wa kumaliza katika nne bora.
Mashabiki wa West Ham wakilishambulia gari la Manchester United kwa makopo ya vinywaji kabla ya mchezo tukio ambalo lilisababisha mchezo huo kuchelewa kuanza.
Askari wakiwatawanya mashabiki wa West Ham
Mafataki yakipigwa baada ya kumalizika kwa mchezo.
.
Paulo Di
Canio
Sir Trevor Brooking
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni