STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatatu, 6 Juni 2016

YANGA TENA YAIPATA SAINI YA BEKI KISIKI WA MTIBWA SUGAR..............

BEKI wa Mtibwa Sugar, Andrew Vincent 'Dante'amesaini Mkataba wa miaka miwili kujiunga na Yanga SC leo hii.
 
Vincent, mmoja wa mabeki wa kati waliofanya vizuri msimu huu amesaini muda mfupi baada ya kusiani kipa wa Prisons, Beno Kakolanya leo. 
  Dante sasa anakwenda kupambana kugombea namba dhidi ya mabeki wengine wa kati wa Yanga, Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro', Kevin Yondan, Pato Ngonyani na Mtogo Vincent Bossou.
  Kakolanya pia amesaini Mkataba wa miaka miwili kujiunga na wafalme hao wa soka ya Tanzania, Yanga SC, jambo ambalo ni pigo kwa mahasimu, Simba SC waliokuwa wanamtaka kipa huyo. 
  Kakolanya anakwenda kuungana na makipa watatu waliopo Yanga, Deo Munishi ‘Dida’, Ally Mustafa ‘Barthez’ na Benedicto Tinocco kufanya idadi ya makipa wanne.
  Hata hivyo, mustakabali wa Tinocco haueleweki sasa baada ya kusajiliwa kwa Kakolanya mwenye umri wa miaka 22, ambaye Prisons ilimuibua Mbaspo Academy.
Picha Bin Zubeir

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox