
Alikuwa Mohammed Rashid Abdallah aliyeindikia Serengeti boys goli la kwanza katika dakika ya 33 goli lilodumu kipindi chote cha kwanza.
Katika dakika ya 44 kiungo wa Serengeti Boys Ng'anzi alizawadiwa kadi nyekundu ikiwa ni baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano.
Kipindi cha pili muda mwingi Serengeti Boys walikuwa wakilinda goli lao na kupeleka mashambulizi ya kushtukiza ambapo katika dakika ya 82 Muksin Makame aliiandikia Serengeti boys goli la pili na kupelekea mchezo kumalizika kwa Serengeti boys kuibuka na ushindi wa goli 2-0.
Matokeo ya leo ukiunganisha na matokeo ya mchezo wa awali uliochezwa Afrika kusini ambapo ulimalizika kwa sare ya goli 1-1, hivyo unaifanya Serengeti boys kuiondosha Afrika kusini kwa jumla ya magoli 3-1.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni