STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 29 Aprili 2018

UBINGWA HUUOOOO MSIMBAZI, WAICHAPA YANGA KAMOJA TU, GEPU ALAMA 14

Klabu ya Simba imeibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya klabu ya Yanga kwenye mchezo wa Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara uliofanyika katika Uwanja wa Taifa leo Aprili 29, 2018 jijini Dar es salaam.
Goli la Simba limefungwa na Erasto Nyoni kunako dakika ya 37 kipindi cha Kwanza kwa makosa ya mabeki wa Yanga.
Hata hivyo mchezo huo ulionekana kuwa sawa kwa timu zote mbili kwani timu hizo zilionekana kushambuliana kwa zamu.
Beki Hassan Kessy alitolewa nje mnamo kipindi cha pili kwa kadi ya pili ya njano na nyekundu kutokana na kitendo cha kumchezea faulo, Asante Kwasi.


Kwa matokeo hayo Simba SC wameendelea kujiimarisha kileleni kwenye msimamo wa VPL kwa alama 62 wakifuatiwa na Azam alama 49 na huku Yanga wakisalia nafasi ya tatu kwa alama 48.

Simba SC; Aishi Manula, Nicholas Gyan, Asante Kwasi, Erasto Nyoni, Yussuf Mlipili, James Kotei, Jonas Mkude, Shomary Kapombe, John Bocco, Emmanuel Okwi na Shiza Kichuya.
Benchi; Said Mohammed 'Nduda', Paul Bukaba, Said Ndemla, Mohammed Hussein 'Tshabalala', Muzamil Yassin, Laudit Mavugo na Rashid Juma.

Yanga SC; Youthe Rostand, Hassan Kessy, Gardiel Michael, Andrew Vincent 'Dante', Kelvin Yondan, Said Juma 'Makapu', Yussuf Mhilu, Papy Kabamba Tshishimbi, Obrey Chirwa, Raphael Daudi na Ibrahim Ajib.
Benchi; Ramadhani Kabwili, Juma Abdul, Abdallah Shaibu 'Ninja', Maka Edward, Juma Mahadhi, Pius Buswita na Emmanuel Martin.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox