STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumatano, 8 Aprili 2015

MAN UNITED YAPANGA KUIONYESHEA ARSENAL JEURI YA PESA KWA CAVANI.

KLABU ya Manchester United inatarajia kuonyesha uwezo wake wa kifedha kwa kuwapiku Arsenal katika kutafuta saini ya mshambuliaji wa Paris Saint-Germain Edinson Cavani. Meneja wa United Luois van Gaal amemfanya Cavani kuwa kinara katika mipango yake ya usajili majira ya kiangazi wakati akijiandaa kuwaruhusu kuondoka Robin van Persie na Radamel falcao aliyekuwa kwa mkopo akitokea AS Monaco. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger pia anataka kumsajili Cavani wakati akijaribu kuimarisha kikosi chake ili kiwe cha ushindani zaidi msimu ujao. Lakini United wanajiamini uwezo wao wa kifedha utawafanya kufanikiwa kumshawishi Cavani kutua Old Trafford katika usajili unaotabiriwa kuwa mkubwa majira ya kiangazi. Inaarifiwa kuwa Van Gaal yuko tayari kutoa ofa ya paundi milioni 60 kwa PSG kwa ajili ya Cavani huku wakipanga kumlipa mshahara wa paundi 300,000 kwa wiki na kumfanya kufikia kiwango cha Wayne Rooney. Cabani mwenye umri wa miaka 28 alijiunga na PSG akitokea Napoli kwa kitita cha paundi milioni 55 mwaka 2013 lakini ameshindwa kung’aa kutokana na kufunikwa na Zlatan Ibrahimovic.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox