STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Alhamisi, 12 Novemba 2015

TIKETI ZA MECHI YA STARS NA ALGERIA KUANZA KUUZWA KESHO.

TIKETI za mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia chini Urusi mwaka 2018 kati ya Tanzania dhidi ya Algeria zitaanza kuuzwa kesho Ijumaa katika vituo 10 viliyopo jijini Dar es salaam. 
 
Magari maalumu yenye stika yataanza kuuza tiketi hizo za mchezo kesho saa 2 kamili asubuhi mpaka saa 12 jioni, ambapo tiketi zinauzwa kwa shilingi elfu tano (5,000) kwa viti vya rangi ya bluu na kijani na rangi ya machungwa, na elfu kumi (10,000) kwa viti vya VIP B & C. 
 
Vituo vitakavyotumika kuuza tiketi hizo ni ofisi za TFF – Karume, Buguruni – Oilcom, Mbagala – Darlive, Mnazi Mmoja, Luther House – Posta, Big Bone – Msimbazi, Ubungo – Oilcom, Makumbusho – Stand ya Daladala, Uwanja wa Uhuru. 
 
TFF inawaomba wadau, washabiki na watanzania kujitokeza kwa wingi kununua tiketi za mchezo huo katika magari maalumu yatakayokuwepo kwenye vituo vilivyotajwa, ili kuondokana na tatizo la kuuziwa tiketi zisizokuwa halali. 
 
Wakati huo huo Ubalozi wa Algeria nchini Tanzania, umewataka waandishi wa habari wanaotrajia kwenda kuripoti mchezo wa marudiano jijini Algiers siku ya jumanne, kuwasilisha maelezo ya chombo wanachofanyia kazi pamoja na vifaa watakavyovitumia kwenye mchezo huo (camera, vinasa sauti) kuwasilisha maelezo hayo leo Alhamsi kabla ya saa 9 mchana katika ofisi za Ubalozi huo kwa ajili ya kupatiwa Accreditation za kufanyia kazi. 
 
Matokeo ya mchezo wa jana Azam Sports Federtaion Cup (ASFC), ni Mshikamano 0 - 1 Cosmopolitan,

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox