MTANDAO mmoja barani 
Ulaya umetoa taarifa kuwa tayari muafaka umeshafikiwa kwa michuano ya 
Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Qatar mwaka 2022 kufanyika katika 
kipindi cha Novemba na Desemba ili kuwepa joto kali katika kipindi cha 
kiangazi. Wakiorodhesha vyanzo mbalimbali mtandao huo umedai kuwa uamuzi
 umeshafanyika kwani kikosi kazi kilichoteuliwa na Shirikisho la Soka 
Duniani-FIFA kinatarajia kuwasilisha miezi hiyo katika kikao chao 
kitakachofanyika wiki ijayo jijini Doha kabla ya kamati ya utendaji 
haijakamilisha mpango huo wakati wa kikao cha mwezi ujao jijini 
Zurich. Wiki tatu zilizopita, katibu mkuu wa FIFA Jerome Valcke katika 
mahoajiano yake na radio moja nchini Ufaransa alisema Kombe la Dunia 
nchini Qatar linatakiwa kuandaliwa wakati wa majira ya baridi lakini 
kugongana na michuano ya olimpiki ya kwenye baridi Februari mwaka 2022 
pia ni hatihati. Hata hivyo mpango huo haujafafanua kwa undani zaidi 
kuwa michuano ya Kombe la Shirikisho ambayo huchezwa mwaka mmoja kabla 
ya Kombe la Dunia kama nayo itasogezwa mbele kuepuka majira ya 
kiangazi. Desemba mwaka jana  Chama cha Vilabu barani Ulaya na Muungano 
wa Ligi za Soka barani humo vilipendekeza michuano hiyo ya Qatar 
kuchezwa kati ya May na Juni ili kutovuruga ratiba zingine za kawaida za
 msimu.
TANGAZA NASI: +255 655 442 255
CHANZI OPEN SCHOOL
Ijumaa, 20 Februari 2015
KOMBE LA DUNIA MWAKA NCHINI QATAR KUFANYIKA NOVEMBA NA DESEMBA MWAKA 2022.
About asantemuya
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA
Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...
TIBA YA KIIMANI
a



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni