STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 22 Mei 2015

HAZARD AFANYIWA UPASUAJI

Nyota wa Chelsea Eden Hazard alishindwa kuhudhuria sherehe ambapo alitakiwa kutunukiwa tuzo ya mchezaji bora msimu kwa waandishi wa habari baada ya kuwa akiuguza majeraha yake yaliyotokana na upasuaji wa fizi aliofanyiwa hivi karibuni.
Hazard ambaye alijinyakulia kura za kutosha kutoka kwa waandishi, huku akipata asilimia 53 na kumzidi Harry Kane wa Tottenham ambaye alishika nafasi ya pili, alitakiwa kukabidhiwa zawadi yake katika sherehe zilizofanyika jijini London.
"Shukrani za dhati ziwafikie Waandishi wa Habari za Michezo nchini Uingereza kwa kunichagua kuwa mchezaji wao wa msimu. Naomba radhi kuwa sitaweza kuhudhuria usiku huu mahala hapo lakini tafadhali mnatakiwa kufahamu kuwa ninajivunia sana juu ya hii zawadi ambayo kwangu mimi ni kubwa sana," aliandika hivyo kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox