STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumamosi, 16 Mei 2015

KOCHA MPYA WA SIMBA MTARAJIWA NI HUYU HAPA


Kocha Piet de Mol raia wa Ubelgiji ndiye atachukua mikoba ya Goran Kopunovic.

De Mol anatarajia kutua nchini kati ya Mei 21 hadi 23 tayari kumaliza na uongozi wa Simba na mara moja ataanza kazi.
Uongozi wa Simba umefikia uamuzi huo baada ya Kopunovic kutaka dau kubwa sana.

Kopunovic aliondoka mapema wiki hii kurejea kwao huku akiwa ameshindwa kuelewana na uongozi wa Simba.

MSerbia huyo anayeishi nchini Hungary alitaka kulipwa dola 50,000 (sh milioni 100) kama ada ya usajili.

Pia alitaka kupewa mshahara wa dola 14,000 ambazo zingemfanya kuwa kocha ghali zaidi nchini.

Simba iliamua kubadili uamuzi wa kubaki naye na kufanya mazungumzo na Mbelgiji huyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox