STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumanne, 19 Mei 2015

MOURINHO BADO AMFAGILIA MESSI, ANGALIA KAULI YAKE NYINGINE KUHUSU MESSI

Mpira wa bara la Ulaya utakuwa na mabadiliko makubwa sana kama ikitokea Lionel Messi anaondoka Barcelona, hii ni kauliya kocha wa Chelsea Jose Mourinho.
Messi amekuwa ni mtu muhimu sana katika klabu ya Barcelona kwa takribani muongo mmoja sasa, akiwasaidia kutwaa makombe matatu ya ligi ya mabingwa Ulaya, makombe sita ya La Liga na mengine kadhaa ambayo hayajatajwa.
Mourinho, ambaye alimpoka taji la La Liga Guardiola mwaka 2012 wakati akiinoa Real Madrid anahisi kuwa Muargentina huyo mwenye umri wa miaka 27 ndio nguzo kubwa ya mafanikio ya klabu hiyo
"Ndani ya kipindi cha miaka 10 ambacho Messi hatokuwepo, ramani ya soka la Ulaya lazima itabadilika sana," Mourinho aliiambia talkSPORT.
"Walichoshinda Barcelona katika miaka kadhaa iliyopita wakiwa ama na Frank Rijkaard, Pep Guardiola au Luis Enrique kama makocha ni kwa sababu wamekuwa na kiumbe huyu."
Chelsea wamewahi kuhusishwa na kumwania Messi, ambaye kwa wakati fulani alionekana kutokuwa na furaha klabuni hapo, lakini Mourinho alikanusha vikali taarifa hizo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox