MICHUANO ya Copa America inatarajiwa kuanza kutimua vumbi leo ambapo wenyeji Chile watakwaana na Ecuador katika mchezo wa ufunguzi utakaochezwa katika Uwanja wa taifa uliopo jijini Santiago.
Akihojiwa kuelekea katika mchezo huo ambao utachezwa majira ya saa nane za usiku kwa saa za hapa nyumbani, kocha wa Chile Jorge Sampaoli amesema amejiandaa vyema kwa ajili ya mchezo huo kwa kuwa anajua ugumu wake.
Sampaoli amesema watu wengi wanawapa nafasi wao na kuwadharau wapinzani wao lakini yeye hataki kubweteka na hilo kwani anaamini kila timu imejiandaa kikamilifu kwa ajili ya mchezo muhimu.
Chile ilifanikiwa kufikia hatua ya robo fainali ya michuano hiyo mwaka 2011 kabla ya kutolewa na Venezuela kea kufungwa mabao 2-1. Mchezo mwingine wa kundi A utazikutanisha timu za Bolivia watakaokwaana na Mexico.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni