STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Ijumaa, 21 Agosti 2015

COASTAL, STAND UNITED NA TOTO AFRICANS ZACHEMSHA USAJILI, FAINI YA TFF INAWAHUSU....

Boniface Wambura, Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi
Dirisha la usajili kwa vilabu vya Ligi Kuu nchini (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) limefungwa jana ambapo vilabu vitatu tu vya VPL vimeshindwa kuwasilisha usajili wao wa wachezaji katika muda uliopangwa.
Klabu za Coastal Union ya Tanga, Stand United ya Shinyanga na Toto African ya jijini Mwanza zimeshindwa kuwasilisha usajili wao wa wachezaji, faini ni laki tano (500,000) kwa kila klabu iliyochelewesha usajili au itakayobadili majina au kuongeza majina baada ya tarehe ya jana.
Awali TFF ilitoa muda wa wiki mbili kwa vilabu vyote nchini kukamilisha usajili, ambapo vilabu 13 vya ligi kuu vimeweza kukamilisha ndani ya wakati, vilabu 24 vya ligi daraja la kwanza, vilabu 24 ligi daraja la pili pia vimeweza kukamilisha usajili wao ndani ya muda uliopangwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox