MENEJA wa Arsenal,
Arsene Wenger amesema ataipa uzito mkubwa michuano ya Europa League kama
waking’olewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Arsenal wako
wanasuasua katika kundi F wakiwa na alama tatu pekee katika michezo
minne waliyocheza na wanatarajiwa kucheza na Dinamo Zagreb baadae leo
wakijuwa kuwa wanaweza kutolewa kama wakifungwa.
Nafasi ya tatu katika
kundi hilo itawapeleka Arsenal katika Europa League na Wenger amesema
hadhani kama kushiriki michuano hiyo kutaathiri dhamira yao ya kupigania
taji la Ligi Kuu.
Akihojiwa Wenger amesema kama kikosi chake
kikienguliwa na kwenda kushiriki michuano hiyo ya pili kwa ukubwa barani
Ulaya basi hakuna kuwa ataipa uziti unaostahiki.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni