KLABU ya Corinthians
wametawadhwa mabingwa wapya wa Brazil jana baada ya sare ya bao 1-1
waliyopata dhidi ya Vasco da Gama na kusaidiwa na kipigo cha mabao 4-2
walichpata Atletico Mineiro dhidi ya Sao Paulo ambacho kimewafanya
kuongoza kwa alama 12 huku zikiw zimesalia mechi tatu.
Corinthians ndio
vinara wa mabao katika ligi na safu imara ya ulinzi huku pia wakiwa
wameshinda mechi nyingi zaidi na kufungwa chache kuliko timu nyingine
yeyote. Klabu hiyo hiyo imenyakuwa taji hilo ambalo ni la sita kwao
wakiwa wanaongoza kwa alama 77 wakati Atletico waliokuwa wakifuatia
wakiwa na alama 65.
Akihojiwa golikipa wa Corinthians aliwapongeza
wachezaji wenzake kwa jinsi walivyojituma na kuongeza kuwa walistahili
taji hilo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni