MENEJA w Arsenal, Arsene
Wenger anataka vipimo bora kwa ajili ya kugundua wachezaji wadanganyifu
katika soka na kutaka vipimo vya damu view vikifanyika mara kwa
mara.
Chama cha Soka Uingereza-FA kilimtaka Wenger mwenye umri wa miaka
66, kufafanua kauli yake aliyotoa kuhusu dawa za kusisimua misuli katika
mahojiano na gazeti moja la Ufaransa.
Kocha huyo raia wa Ufaransa
amesema yuko tayari kuzungumza na FA kwasababu anataka vipimo vifanyike
kwa undani zaidi na juu juu kama hivi sasa ili kuweza kulikabili vyema
tatizo hilo.
Kiungo wa Dinamo Zagreb, Arijan Ademi alishindwa vipimo
kufuatia mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya walioshinda dhidi ya Arsenal
Septemba mwaka huu.
Na Wenger akihojiwa kuelekea mchezo wao wa kesho wa
Ligi Kuu dhidi ya West Bromwich Albion, amesema ni ujinga kudhani soka
halina masuala ya matumizi ya dawa za kusisimua misuli kama michezo
mingine.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni