Mchezaji tenisi namba moja Duniani kutoka Serbia, Novak Djokovic amemaliza msimu wake kwa ushindi dhidi ya Roger Federer.
Djokovic alifanikiwa kushinda kwa seti 6-3, 6-4 katika dakika 80 za mchezo huko London, na aliweza kusahihisha makosa yake baada ya mechi ya mwanzo ya makundi kufungwa na Roger Federer.
Mpaka sasa Djokovic anamaliza mwaka huu kwa kushinda mataji 11 yakiwemo ya matatu ya Gland slam, na kwa upande wake Roger Federer amesema hakuna furaha yoyote katika upande ulioshindwa ila ni vizuri kushiriki kuliko kutoshiriki kama mwaka uliopita.
Gwiji wa Arsenal na mchambuzi wa kituo cha Sky Thierry Henry akiwa na modo wa Bosnia Andrea Rajacic kwenye fainal ya Djokovic na Federer
Mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud akiwa miongoni mwa mastaa waliohudhuria mchezo huo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni