Ronaldinho alishangiliwa na mashabiki wa Real Madrid 19-11-2005, kwenye mchezo uliofanyika
Bernabeu kutokana na umaridadi alioonesha.
Katika mchezo huo ambao Barcelona walishinda kwa magoli 3-0 huku Ronaldhinho akifunga miongoni mwa magoli bora kabisa katika mechi za El clasico.
Ikiwa ni miaka kumi tangu tukio hilo la kusisimua litokee hapo jana mashabiki wa Real Madrid wakafanya kama walivyo fanya 2005 kwa Ronaldinho baada ya kumshangilia Iniesta alipokuwa anatoka dakika ya 77 kumpisha Messi.
Shangwe hizo ni kutokana na kiwango bora kabisa alichoonesha dhidi ya Real Madrid waliofungwa magoli 4-0
Ronaldinho alipokuwa Barcelona 2005
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni