SHIRIKISHO la Soka la
Ulaya-UEFA, limebainisha kuwa mechi zake za Ligi ya Mabingwa Ulaya na
Europa League zitaendelea kama zilivypangwa wiki ijayo.
Ratiba ya
michezo mingi ilisimamishwa au kusogezwa mbele maeneo mengi ya Ulaya
kufuatia mashambulio ya kigaidi yaliyofanyika jijini Paris Ijumaa
iliyopita.
Mchezo wa kirafiki kati ya Ujerumani na Uholanzi uliokuwa
uchezwe jijini Hannover Jumanne nao ulifutwa dakika za mwisho baada ya
taarifa za kuwepo kwa tishio la bomu.
Msemaji wa UEFA amesema shirikisho
hilo linafanya kazi kwa karibu na klabu zitakazokuwa nyumbani pamoja na
mamlaka husika ili kuhakikisha taratibu muhimu zinafuatwa kuhakikisha
usalama wa watu wote.
Msemaji huyo aliendelea kudai kuwa bado
hawajalijadili suala la mashabiki watakaosafiri kwani hilo linahusu
mamlaka husika kutoa maamuzi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni