WACHEZAJI na mashabiki
watakaohudhuria mchezo wa mwishoni mwa wiki wa Clasico kati ya Real
Madrid na Barcelona katika Uwanja wa Santiago Bernabeu watasimama kwa
dakika moja kutoa heshima kwa wahanga wa tukio la mashambulio ya kigaidi
jijini Paris.
Mchezo huo unaozikutanisha klabu hasimu katika La Liga
unakadiriwa kutizamwa na watu zaidi ya milioni 500 ikiwa ndio mechi ya
vilabu inayotizamwa zaidi duniani.
Katika taarifa iliyotolewa imedai
kuwa kutakuwa na dakika moja za kukaa kimya kuwakumbuka wahanga hao
kabla ya kuanza kwa mchez huo wa Jumamosi ambao utahudhuriwa na watu
81,000.
Wakati wa kukaa kimya dakika moja klabu zote zitakuwa na mabango
yenye maandishi yanayosomeka kuwa Sisi Sote Ni Wafaransa ambayo pia
yataonekana katika picha za video kwa wale wasiokuwepo uwanjani.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni