STAY WITH US

LightBlog

Breaking

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

TANGAZA NASI: +255 655 442 255

CHANZI OPEN SCHOOL

CHANZI OPEN SCHOOL

Jumapili, 29 Novemba 2015

ZAMA ZA VLADIMIR KLITSCHKO ZAMALIZWA NA TYSON FURY

BONDIA Tyson Fury ndiye bingwa mpya wa ndondi za kulipwa uzito wa juu, baada ya kumdunda Wladimir Klitschko katika pambano kali la kihistoria.
 
Muingereza Tyson Fury amemshinda Wladimir Klitschko wa Ukraine kwa pointi usiku wa jana mjini Dusseldorf, Ujerumani na kijana huyo wa umri wa miaka 27 anabeba mataji yote makubwa ya ngumi uzito wa juu, WBA, IBF na WBO.
 
Fury hakumpa nafasi Klitschko ya kufurukuta ulingoni kutokana na kumsukumia makonde mfululizo akitumia mikono na mitindo yote kiasi cha 'kumharibu sura' mpinzani wake huyo aliyekuwa mbabe wa ndondi za uzito wa juu kwa karibhu muongo wote huu.
 
Baada ya kumdunda mbabe wa muda mrefu wa ndondi za uzito wa juu, Wladimir mwenye umri wa miaka 39, sasa Fury anatarajia kupambana na Mmarekani, Deontay Wilder anayeshikilia taji la WBC.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KAMATI YA TUZO IMEFANYA MCHUJO KWENYE WACHEZAJI 30 WAMEBAKI 15, MKUDE, AJIBU WAMETOLEWA, ANGALIA ORODHA

Kamati ya Tuzo za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), iliyokutana wiki hii imeteua wachezaji 15 kwa ajili ya kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa VPL msi...

TIBA YA KIIMANI

TIBA YA KIIMANI

a

a
Adbox